13 Desemba 2014

TRA: Watumishi waliotajwa kashfa ya escrow wako kazini

Dar es Salaam. Watumishi wawili wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), waliotajwa katika kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow wanaendelea na kazi wakisubiri taratibu za utumishi wa umma kabla ya kuchukuliwa hatua.
Akizungumza na mwandishi wetu kuhusu hatua zilizochukuliwa baada ya agizo la Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba kutaka wafukuzwe, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo alisema jana kwamba hawajachukuliwa hatua hadi taarifa za uchunguzi za vyombo vya dola itakapotolewa.
Watumishi wawili, mmoja alitajwa katika taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), kutokana na matokeo ya ukaguzi maalumu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kuhusu kashfa hiyo kwamba aliingiziwa Sh1.6 bilioni bila maelezo.
Mwingine katika kashfa hiyo, badala ya kuandika Dola za Marekani 6 milioni aliandika Sh6 milioni na badala ya kuandika Dola za Marekani 20 milioni, aliandika Sh20 milioni.
Kutokana na taarifa hizo wakati wa mkutano wa Bunge wa 16 na 17 uliomalizika hivi karibuni, Mwigulu aliagiza mtumishi wa mamlaka hiyo aliyepata mgawo wa Sh1.6 bilioni kutoka katika Akaunti ya Tegeta Escrow afukuzwe kazi jamba ambalo TRA imesema litatekelezwa baada ya vyombo vya dola kufanya uchunguzi.
Jana, Mwigulu alisema kuwa Kamishna wa TRA amemweleza kuwa kinachofanyika hivi sasa ni kufuata taratibu za utumishi wa umma ili kuwapa watumishi hao nafasi ya kujieleza.
Alisema kutokana na hali hiyo pamoja na taratibu hizo kufuatwa watafikia tu katika maagizo yake aliyoyatoa bungeni.
Akizungumzia agizo lake kwa wale ambao walipata mgawo wa escrow kuwataka walipe kodi kabla ya kufika Desemba 31 mwaka huu, Mwigulu alisema msimamo wa Serikali uko palepale kwamba wasipofanya hivyo watachukuliwa hatua kali.
“Nimezungumza na Kamishna wa TRA leo (jana) amenieleza watawapelekea fomu za kodi wajaze kwa ajili ya kulipa, hivyo msimamo uko palepale kwamba watalipa hiyo kodi,” alisema Mwigulu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728