25 Desemba 2014

Kambi ya jeshi la AU yavamiwa Somalia

Wapiganaji wa Al shabaab wamefanya shambulizi katika kambi kuu ya jeshi la Umoija wa Afrika karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu Somali.

Milipuko na milio ya risasi ilisikika ndani ya kambi hiyo kulingana na kanali Ali Houmed aliyezungumza na shirika la habari la AFP.
Alshabaab imekiri kutekeleza shambulizi hilo na kwamba wapiganaji wake wako ndani ya kambi hiyo.
Jeshi la African Union lina zaidi ya wanajeshi 20,000 nchini humo ili kuisadia serikali ya Somali kukabiliana na Al-shabaab.
Wapiganaji wa Alshabaab
Sheikh Abdiasis Abu Musab,ambaye ni msemaji wa kundi la Alshabaab amesema kuwa wapiganaji wa kundi hilo waliingia kwa nguvu ndani ya kambi hiyo.
Wapiganaji wetu wameingia katika kambi hiyo ya Halane kwa nguvu kupitia lango kuu na sasa mapigano yanaendelea ndani ya kambi hiyo.
Kambi hiyo ya jeshi iko karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu.
Kambi hiyo pia ni makao ya balozi za Uingereza na Italy na hutumiwa kama makao makuu ya operesheni za umoja wa mataifa nchini Somali.
Aleem saddique ,ambaye ni msemaji wa umoja wa mataifa nchini somali ameikiambia chombo cha habari cha Reuters kwamba wafanyikazi wote wa umoja wa mataifa wako salama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728