02 Machi 2016

Mtaala mpya wa madereva wa pikipiki wazinduliwa TZ


Kufuatia ongezeko la visa vingi vya ajali barabarani ,taasisi ya kitaifa ya uchukuzi NIT pamoja na Mamlaka ya uchukuzi wa ardhini na baharini Sumatra zimezindua mtaala mpya wa kuwafunza madereva wa pikipiki.
Idadi ya pikipiki nchini Tanzania imeongezeka kutoka 308,412 mwaka 2010 hadi 1,047,659 kufuatia kuimarika kwa biashara ya pikipiki.
Ukuaji huo hatahivyo umekuwa na athari kubwa za ajali za barabarni huku data iliotolewa na
kamanda wa idara ya trafiki nchini Tanzania Mohammed Mpinga ikionyesha kuwa ajali zinazohusishwa na pikipiki ambazo hutumika kwa uchukuzi hushirikisha asilimia 60 ya jumla ya wagonjwa wanaolazwa katika hospitali kuu ya Muhimbili.
Nchini Tanzania ajali za barabarani ziliwaua takriban watu 3,468 mwaka 2015,ambapo ajali zinazohusisha pikipiki ziko katika nafasi ya tatu kwa kusababisha vifo nchini humo baada ya HIV na Malaria.
Mpinga hatahivyo amesema kuwa pikipiki zitaimarisha viwango vya usalama barabarani kupitia kuvaa kofia za helmet,kutobeba zaidi ya mteja mmoja mbali na kutokunywa pombe wakati mtu anapoendesha.
Vilevile amewaonya wale wanaohusika katika uhalifu akisisitiza usajili wa pikipiki kote nchini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728