01 Machi 2016

Watafutaji kazi walazimishwa kuvua nguo India


Mamia ya vijana katika jimbo la Bihar nchini India wamelazimishwa kuvua nguo ili kusalia na suruali zao za ndani wakati wa mtihani wa kuajiriwa kwa wanajeshi ili kuzuia kufanyika kwa udanganyifu.
Picha zimeonyesha vijana wanaowania kuwa wanajeshi wakiwa wamekaa na kukunja miguu katika uwanja mmoja ulopo mji wa Muzaffar huku wakiwa wamevalia suruali zao za ndani pekee.
Jeshi limesema kuwa lilifanya hivyo ili kuhifadhi mda wa kuwachunguza makurutu wengi.

Kurutu mmoja aliliambia gazeti la India Express alihisi kwamba hawakupewa heshima.
Maafisa wanasema kuwa makurutu wapatao 1,159 walishiriki katika mtihani huo wa saa moja wa kujiunga na jeshi la India.
''Wakati tulipoingia katika eneo la Chakkar Maidan,tuliagizwa kuvua nguo zote isipokuwa suruali ya ndani.Hatukuweza kukataa bali kutimiza yaliohitajika licha ya kwamba halikuwa jambo la kawaida''.
Makurutu hao walitawanywa kwa urefu wa futi nane kila upande,Gazeti la India Express lilimnukuu kurutu mmoja akisema.
Gazeti hilo lilimnukuu afisa mmoja wa ngazi za juu katika jeshi akisema kuwa ni makosa kwa utawala kuwafanyia hivyo makurutu hao.
Bihar na maeneo mengine ya India Kaskazini ni maarufu kwa udanganyifu katika mitihani ,mwaka uliopita serikali ya jimbo hilo iliaibishwa baada ya wazazi na marafiki kupigwa picha wakipanda kuta za shule ili kuwapatia majibu ya mitihani wanafunzi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728