Gazeti moja nchini Israel limeripoti kuwa wataaamu kutoka kwa kampuni hiyo ya Cellebrite wanahusika katika kesi hiyo.
Maafisa wa Cellebrite wameambia BBC kwamba huwa wanafanya kazi na FBI lakini hawakueleza zaidi.
Tovuti ya kampuni hiyo hata hivyo inasema miongoni mwa mengine kampuni hiyo ina uwezo wa kufungua na kupata habari kutoka kwa simu aina ya iPhone 5C, muundo ambao ni sawa na wa simu hiyo ya Farook.
Kampuni ya Apple, inayotengeneza simu za iPhone, imekataa kuwasaidia FBI kuifungua.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni