24 Machi 2016

Waisraeli huenda wanasaidia FBI kufungua simu

SimuKampuni moja inayohusika katika masuala ya ya usalama mtandaoni kutoka Israel inakabilwia na shinikizo la kuitaka ieleze iwapo inasaidia idara ya uchunguzi wa jinai ya Marekani kufungua simu ya iPhone.
Idara ya FBI ilisema Jumatatu kwamba huenda imefanikiwa kupata njia ya kufungua simu ya muuaji Syed Rizwan Farook aliyewapiga risasi watu katika eneo la San Bernardino, California, mwezi Desemba.
Gazeti moja nchini Israel limeripoti kuwa wataaamu kutoka kwa kampuni hiyo ya Cellebrite wanahusika katika kesi hiyo.

Maafisa wa Cellebrite wameambia BBC kwamba huwa wanafanya kazi na FBI lakini hawakueleza zaidi.
Tovuti ya kampuni hiyo hata hivyo inasema miongoni mwa mengine kampuni hiyo ina uwezo wa kufungua na kupata habari kutoka kwa simu aina ya iPhone 5C, muundo ambao ni sawa na wa simu hiyo ya Farook.
Kampuni ya Apple, inayotengeneza simu za iPhone, imekataa kuwasaidia FBI kuifungua.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728