02 Machi 2016

Waliomuasi Kagame kufungwa miaka 22 jela


Aliyekuwa mlinzi wa rais Paul Kagame na mshirika wake wanakabiliwa na hukumu ya miaka 22 gerezani kwa kupanga njama dhidi ya kiongozi huyo wa Rwanda.
Afisi ya kiongozi wa mashtaka nchini Rwanda imeitaka mahakama iwahukumu kifungo cha miaka 22 kanali Tom Byabagamba aliyeiongoza kikosi cha kumlinda rais , na brigedia mstaafu jenerali Frank Rusagara kwa makosa ya kuchochea uma dhidi ya rais Kagame.
Maafisa hao wakuu jeshini walikamatwa mnamo mwezi Agosti 2014.

Wamekanusha madai dhidi yao.
Kiongozi huyo wa Mashtaka alisema mahakamani kuwa Brig-jenerali Rusagara alisikika akiituhumu serikali ya Rwanda kuwa "taifa linalotawaliwa kiimla na kuwa ni taifa lililofeli'
Aidha alidai kuwa '' bwana Kagame ni kiongozi wa kiimla''.
kanali Byabagamba anatuhumiwa kwa kudai kuwa kundi la wapiganaji wa kihutu wa FDLR, waliotekeleza mashambulizi mengi katika taifa jirani la jamhuri ya Congo hawakuwa tishio kwa rwanda.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728