23 Machi 2015

Houthi wateka maeneo zaidi Yemen

Maafisa wa usalama nchini Yemen wanasema waasi wa kundi la Houthi wameshikilia maeneo kadhaa ya mji wa tatu kwa ukubwa wa Taiz, ukiwemo uwanja wa ndege.
Taiz ni mji ambao unapakana na mji mkuu wa Sanaa na mji wa kusini wa Aden.
Umekuwa ni mji ambao una vikosi vitiifu kwa rais Abd Rabbuh Mansour Hadi.

Baraza la usalama la umoja wa mataifa linatarajia kukutana kwa dharura hii leo kujadili kuzorota kwa usalama nchini Yemen, ambako waasi wa Houthi wanatawala eneo kubwa la nchi.
Kikao hicho cha baraza la usalama kimeombwa kuitwa na rais Hadi ambaye mwezi uliopita alikimbilia mjini Aden kutoka mji mkuu wa Sanaa.
Awali wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilitangaza kuwaondosha maafisa wake mia moja waliosalia nchini Yemen kwa sababu za kiusalama.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728