01 Machi 2015

Yanga yasonga mbele michuano ya Afrika

Timu ya Young Africans maarufu kama Yanga ndiyo timu pekee ya Tanzania iliyobakia katika michuano ya Shirikisho la Kandanda barani Afrika, CAF kwa mwaka 2015.

Yanga wameweza kusonga mbele kwa kuwaondoa BDF XI ya Botswana kwa kuwacharaza jumla ya mabao 3-2.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijiji Dar es Salaam, Tanzania, wiki mbili zilizopita Yanga waliwafunga BDF XI magoli 2-0
Timu hizi ziliporudiana mjini Gaborone, Botswana, Ijumaa usiku, BDF XI waliibuka na ushindi wa magoli 2-1.
Hata hivyo ushindi huo haukuwasaidia kwani walijikuta wanatolewa katika mashindano kwa kufungwa jumla ya mabao 3-2.
Sasa Yanga itacheza na timu ya FC Platinum ya Zimbabwe katika hatua inayofuata. FC Platinum iliitoa Sofapaka ya Kenya.
Timu ya Azam iliyopata ushindi mzuri wa mabao 2-0 dhidi ya El Mereikh ya Sudan, katika kinyang'anyiro cha klabu bingwa barani Afrika ilijikuta ikipoteza mchezo wa marudiano mjini Khartoum baada ya kulazwa mabao 3-0 na hivyo El Mereikh kufuzu kwa jumla ya mabao 3-2.
Timu nyingine za Tanzania Zanzibar za KMKM na Polisi zimejikuta zikitupwa nje ya michuano ya vilabu barani Afrika kwa kupoteza michezo yao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728