21 Machi 2015

Tanzania yapitisha muswada wa ajira

Bunge la Tanzania limepitisha muswada wa sheria ya udhibiti wa ajira za wageni wa mwaka 2014 ,ambapo pamoja na mambo mengine unaainisha vipengele muhimu vya ajira kwa wageni na wazawa.Hata hivyo bunge hilo limesisitiza serikali kupitia taarifa za waomba ajira wageni ili kubaini uwezo kuhusu ajira wazoomba na mienendo yao kijamii.
Sheria hiyo pia inawataka watanzania kuwepo katika ajira zote kutokana na sifa zao.huku wageni wakianishiwa aina ya ajira kulingana na mahitaji ili kuleta ushindani sahihi katika soko la ajira nchini humo.

Sheria hiyo inalenga kuvutia waombaji wenye ujuzi kutoka nje kulingana na mahitaji,huku pia ikitoa fursa kwa wazawa.Akichangia muswada huo kabla ya kupitishwa mbunge wa Karatu Yohana natse anaeleza jinsi wazawa wanavyopaswa kunufaika zaidi
Gaudensia Kabaka ni waziri wa kazi na ajira wa Tanzania na hapa amesema kuwa vibali vya kazi kwa wageni na suala la uraia kwa mjibu wa sheria hiyo ni mambo ambayo hayataenda pamoja,bali kinachotakiwa ni kutumiza masharti yote mawili.
Kupitia muswada huu,bunge limesema kuwa ni moja ya hatua itakayosaidia ajira wa vijana wa Tanzania ambayo baadhi yao wanakosa ajira kutokana na mazingira ya kipaumbele kuwa kwa wageni na si wazawa kama ilivyo katika mataifa mengi duniani ambayo kutoa fursa kwa wenyeji na kisha wageni baadaye.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728