01 Machi 2015

Serikali na waasi kuafikiana Mali

Mali
Serikali ya Mali na makundi sita ya wanamgambo wanatarajiwa kutia sahihi makubaliano ya amani yenye nia ya kuleta utulivu nchini humo.

Chini ya makubaliano hayo wanamgambo hao watajumuishwa kwenye jeshi la Mali na kutumwa eneo la kaskazi mwa nchi .
Vikosi vya ufaransa na vingine kutoka nchi za Afrika vilingia nchini Mali mwezi Januari mwaka 2013 kuzuia kuenea kwa wanamgambo walio na uhusiano na mtandao wa al Qaeda kwenda maeneo ya kusini .
Wanamgambo hao walitimuliwa kutoka miji iliyo kaskazini mwa nchi lakini hata hivyo wale walio wafugaji wa Tuareg na makundi mengine ya kiislamu bado yanaendelea na harakati zao.
Kusainiwa makubaliano hayo kunafanyika baada ya baraza la usalama la umoja wa mataifa kutoa vitisho vya vikwazo kwa waasi wa Tuareg na makundi yanayoiunga mkono serikali.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728