23 Machi 2015

Ulimwengu waomboleza kifo cha Lee Yew


Waziri mkuu mwanzilishi wa Singapore, Lee Kuan Yew amefariki dunia.
Lee amefariki akiwa na umri wa miaka tisini na mmoja kutokana na ugonjwa wa mapafu.
Kwa miongo mitatu ya utawala wa Lee alifanikiwa kuipitisha nchi yake katika kipindi cha mpito na kuleta mabadiliko makubwa
ya kiuchumi hasa katika usafirishaji majini kwa kutumia rasilimali kidogo walizokuwa nazo na sasa kuwa kitovu kikubwa cha kibiashara cha kimataifa.

David Adelman ni balozi wa zamani wa Marekani nchini humo, ametuma salamu zake za rambi rambi.
Kifo cha Lee ni mwisho wa enzi zake.
mwisho wa mwanamume mwenye nguvu ya ushawishi aliyeingia madarakani katikati ya miaka ya sitini .
Lee alifanikiwa kuanzisha ushirikiano wa kirafiki kati ya nchi yake na Marekani ambao umedumu hata leo
na unaweza kuvuka mipaka sio kwa singapore tu bali hata kwa watu wa Asia ya kusini Mashariki.
Viongozi mbalimbali duniani wanaendelea kutuma risala za rambirambi kwa Singapore, baada ya kifo cha Lee Kuan Yew hospitalini.
Yew aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 91 baada ya kuugua homa ya mapafu.
Nchini Uchina, wizara ya mashauri ya nchi za kigeni imemsifia na kumtaja Lee Kuan Yew, kama kiongozi wa kipekee wa bara Asia.
Marehemu Lee ambaye aliiletea mabadiliko makubwa taifa la Singapore na kuwa na mojawepo ya bandari maarufu zaidi Duniani huku uchumi wa nchi hiyo ukiimarika maradufu, atasalia katika kumbukumbu la taifa hilo.
Mwanawe ambaye ni waziri mkuu wa sasa nchini humo, Lee Hsien Loong, anasema kuwa Singapore haitawahi kuwa na mtu kama huyo tena.
Katika risala zake za rambirambi, Rais Barrack Obama wa Marekani amemtaja kama gwiji wa historia.
Nchini Uchina, wizara ya mashauri ya nchi za kigeni imemsifia na kumtaja Lee Kuan Yew, kama kiongozi wa kipekee wa bara Asia.
Naye waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, anasema kuwa Bwana Lee alikuwa mmojawepo wa viongozi wakuu duniani.
Serikali ya Singapore imetangaza siku sita ya maombolezo, hadi atakapozikwa siku ya Jumapili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728