02 Juni 2015

Askari watoto wasajiliwa Islamic State

Watoto waliosajiliwa na wapiganaji wa Islamic State wakiswali
Picha za video katika simu ya mkononi ambazo BBC imezipata zinaonekana kuwaonyesha wapiganaji wa Islamic State wakimtesa mvulana wa Syria mwenye umri wa miaka 14.

Picha hiyo ambayo ilipigwa na mpiganaji aliyeasi kutoka kikundi hicho, inaonyesha mvulana huyo akipigwa wakati amefujngwa mikono yake.
Umoja wa Mataifa umeishutumu IS na makundi mengine yenye silaha nchini Syria na Iraq kwa kuwatesa na kuwaua watoto.
Watoto walisajiliwa, kufunzwa na kutumiwa katika uwanja wa vita.
Kijana mwingine ameiambia BBC namna alivyopigana na kuua kwa ajili ya kikundi cha al-Nusra Front chenye uhusiano na al-Qaeda. Wakati huo alikuwa na umri wa miaka 15 tu na wakati huo alipojiunga na IS alimkuta kijana wa miaka 13 akifundishwa itikadi kali ya kidini.
Mvulana wa Syria akiadhibiwa na mpiganaji wa IS
Picha ya simu ya mkononi inamwonyesha Ahmed akiwa amening'inizwa mguu juu.
Amefungwa kitambaa usoni, na wanaume wawili wakiwa wameficha sura zao, wakiwa wamevaa nguo nyeusi kutoka juu hadi chini ya vidole vya miguu. Mmoja ana kifu na bastola na mwingine ana hangaika chumbani akiwana bunduki aina ya AK-47.
Ndani ya maeneo waliyojitangzia kuyatawala, Islamic State imeondoa mfumo wa elimu ya kawaida na badala yake kuanzisha shule za mtindo wa kijeshi ambazo zinawafundisha watoto iutikadi kali ya kidini na kuwafundisha kuua.
Islamic State wamekuwa wakiua nchini Syria na Iaraq, lakini madhara yake yataonekana zaidi baadaye.
Huu ni ufisadi wa karne. Watoto wa IS watakua kuwa watu wazima wakiwa wamefundishwa kuua na kujaa chuki na watazisumbua Syria na Iraq kwa miaka mingi ijayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728