11 Juni 2015

Watalii 8 'walisababisha' tetemeko la ardhi

Mlima Kinabalu
Raia wanne wa kigeni wamefikishwa mahakamani nchini Malaysia kwa kusababisha tetemeko la ardhi.

Raia hao wa kigeni wanatuhumiwa kujipiga picha wakiwa uchi juu ya mlima mrefu zaidi nchini humo jambo lililowakasirisha miungu wao waliosababisha tetemeko hilo lililotimia vipimo vya 5.9 kwenye vipimo vya Richter.
Watalii wakiokolewa katika mlima Kinabalu baada ya tetemeko la ardhi
Kisa hicho kimefanyika kabla ya tetemeko la ardhi kutokea katika mlima huo wa, Kinabalu na kuwauwa wakweaji milima kumi na nane.
Baadhi ya raia wa eneo hilo wanalaumu janga hilo la tetemeko la ardhi kwa matendo ya raia hao ambao wameshtumiwa kutoheshimu mila na tamaduni za wageni hususan kwasababu mlima huo ni mtakatifu.
Maafisa wa serikali wangali wanawatafuta watu wengine 6 wanaokabiliwa na tuhuma zizo hizo.
Bendera ya Malaysia ikipaa karibu na mlima Kinabalu
Miongoni mwa wale ambao tayari wamefikisha mahakamani ni mwanamke mmoja mwingereza na raia wengine wawili kutoka Canada na mmoja mholanzi.
Mlima Kinabalu wenye kina cha futi elfu kumi na tatu ni maarufu sana miongoni mwa watalii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728