20 Juni 2015

Muuaji wa kanisani Charleston ashtakiwa

Mshukiwa wa mauaji ya kanisani nchini Marekani ameshtakiwa na mashtaka tisa ya mauaji
Mshukiwa wa mauaji ya watu tisa katika kanisa la kihistoria la Kiafrika katika mji wa Charleston ameshtakiwa na mashtaka tisa ya mauaji pamoja na
shtaka moja la kumiliki silaha, polisi wamesema.
Mshukiwa Dylan Roof mwenye umri wa miaka 21,anatarajiwa kufikishwa kwa mara ya kwanza mahakamani baadaye hii leo kupitia teknolojia ya video.
Polisi wanayachukulia mauaji hayo katika kanisa la Emanuel AME siku ya jumatano usiku katika mji wa kusini mwa Carolina kama uhalifu wa chuki.
Alikamatwa siku iliofuata yapata maili 200 kutoka mji wa Carolina kazkazini kabla ya kusafirishwa na kurudishwa mjini Charleston.
Gavana wa jimbo la Carolina Kusini Nikki Haley amesema kuwa bwana Roof anapaswa kupewa adhabu ya kifo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728