02 Juni 2015

Liverpool yajizatiti kumnasa Milner

Timu ya Liverpool iliyo katika ligi kuu ya England nchini Uingereza imeanza harakati za kusaka wachezaji watakaoisaidia kufanya vizuri katika ligi kuu hiyo.

Liverpool ambayo msimu uliomalizika ilionekana kuwa moja ya timu ambazo zingeleta ushindani mkubwa katika kuwania nafasi nne za juu katika ligi kuu hiyo ilijikuta ikiangukia nafasi ya sita.Katika kuimarisha kikosi chake msimu ujao, Liverpool wamejipanga kufanya mazungumzo na mchezaji wa Manchester City, James Milner wiki hii wakati wakikaribia kunasa sahihi ya mchezaji huyo kiungo akiwa mchezaji huru.
Klabu hiyo ya Anfield imempa kipaumbele mchezaji huyo wa kimataifa wa England.
Liverpool inajiamini kuwa itafikia makubaliano na Milner mwenye umri wa miaka 29.
Iwapo mkataba huo utakamilika, Milner - ambaye alijiunga na Manchester City akitokea Aston Villa mwaka 2010 - atajiunga na Wekundu hao tarehe Mosi mwezi ujao.
Milner alianza kuichezea timu ya taifa ya England dhidi ya Uholanzi mwezi Agosti 2009 na amebaki mchezaji wa kutegemewa katika kikosi cha Roy Hodgson.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728