02 Julai 2015

Mshambuliaji wa Tunisia alikuwa Libya

Mshambuliaji wa Tunisia
Seifeddine Rezgui alipokea mafunzo ya itikadi kali wakati akisomea shahada ya uhandisi
Seifeddine Rezgui, mshambuliaji wa Tunisia aliyewaua watu 38 katika mgahawa wa kifahari eneo la Sousse anaaminika kupata mafunzo ya vita nchini Libya.

Wizara ya ndani imesema kwamba Rezgui amekuwa nchini Libya tangu mwezi Januari sawa na wanaume wawili walioshambulia makavazi mjini Tripoli mwezi Machi. Wengi waliouawa kwenye shambulio la Sousse ni watalii wakiwemo Waingereza 30.
null
Waathiriwa wengi wa shambulio hilo walikuwa watalii
Kundi la Islamic State limekiri kuhusika na shambulio hilo.Rezgui alipata mafunzo ya itikadi kali wakati akisomea shahada ya uhandisi.
Tayari maafisa wa Tunisia wamewakamata washukiwa kadhaa wanaodaiwa kushirikiana na mshambuliaji huyo. Rais wa Tunisia Beji Caid Essebsi amekiri kwamba maafisa wa usalama hawakutarajia shambulio kama hilo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728