16 Julai 2015

Mahujaji 27 waaga dunia India

Zaidi ya mahujaji 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India.
Zaidi ya mahujaji 27 wameuawa kufuatia mkurupuko uliotokea katika warsha moja ya kidini katika jimbo la Andhra Pradesh nchini India.

Mkanyagano huo ulitokea wakati wa kuanza kwa sherehe za Maha Pushkaralu ambapo maelfu ya watu waliokuwa wamekusanyika kuoga kwenye maji ya mto Godavari walianza kusukumana.
Mkurupuko huo ulitokea mwendo wa saa nane u nusu katika mji wa Rajahmundry
Polisi wanasema kuwa umati ulikimbia kwenda kwa lango la kuinga mtoni.
Mikurupuko kama hii hutokea kwa wingi wakati wa warsha za kidini nchini India ambapo watu wengi hung'ang'ania nafasi katika maeneo madogo.
null
Mikurupuko kama hii hutokea kwa wingi India
Waandalizi wanasema kuwa takriban watu milioni 24 wanatarajia kushiriki katika hafla hiyo inayotarajiwa kudumu kwa siku 12.
Mahujaji hao wa dini hiyo wanaamini kuwa kuoga na maji ya mto huo huosha mtu madhambi yake.
Waziri mkuu wa jimbo hilo Andhra Pradesh bwana Chandrababu Naidu, alisema kuwa inahuzunisha mno kuwa mahujaji waliokuwa wakitarajia kuosha madhambi yao wanaangamia.
Mwaka wa 2013 watu 115 walipoteza maisha yao katika mkurupuko uliotokea katika hafla ya kidini ya wahindu katika jimbo la Madhya Pradesh

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728