28 Julai 2015

Kampuni ya simu bandia za iphone yavamiwa

Iphone
Kampuni iliyodaiwa kutengeneza simu bandia 41,000 aina ya Iphones kutoka kampuni ya Apple imevamiwa huko Uchina na watu 9 kukamatwa.

Oparesheni hiyo ilishirikisha mamia ya wafanyikazi waliokuwa wakiandaa vipuri vya simu vilivyotumika kama simu mpya aina ya iphone tayari kuuzwa nje,huku simu hizo bandia zikizalisha kitita cha dola miloni 19.
Kampuni hiyo iligunduliwa tarehe 14 mwezi Mei lakini ikabainika katika mitandao ya kijamii na ofisi ya usalama ya umma Beijing siku ya jummapili.
Oparesheni hiyo ilianzishwa mwezi wa januari.
Uchunguzi huo uliongozwa na kundi la mke na mumewe kaskazini mwa mji mkuu wa Uchina, kulingana na mamlaka ya Beijing.
Walisema kuwa walidokezewa na mamlaka ya Marekani ambayo ilinasa simu hizo bandia .
Ripoti hiyo inajiri wakati kuna msako wa bidhaa bandia unaotekelezwa na Uchina huku mamlaka hiyo ikiyashinikza makampuni kuweka nembo za ubora wa biadha.
Uchina pia imekubali kufanya kazi na mamlaka ya Marekani kupunguza kuwepo kwa bidhaa bandia zinazotoka nchi hizo mbili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728