06 Julai 2015

Viongozi wajadili mzozo wa Burundi

Ghasia zimesababisha maelfu ya watu kuitoroka nchi hiyo
Ni mkutano wa tatu wa dharura kujadili mzozo na mkwamo wa kisiasa nchini Burundi uliosababisha maelfu ya raia kuitoroka nchi hiyo.

Viongozi hao wakiwemo mwenyekiti na mwenyeji wa jumuiya, rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, na Yoweri Museveni wa Uganda, ambao tayari wamewasili kwenye kikao hicho, wanajadili na kuwasilisha mapendekezo ya ripoti mbili kuhusu mgogoro wa Burundi.
Ripoti hizo ni pamoja na ya kikosi cha pamoja cha kimataifa cha Usuluhishi wa mgogoro wa Burundi, kinachojumuisha, Umoja wa Afrika, na Umoja wa mataifa, jumuiya hiyo ya Afrika mashariki, pamoja na kikosi cha kimataifa kuhusu eneo la maziwa makuu. Pamoja na ripoti ya baraza la mawaziri wa Afrika Mashariki.
null
Rais Nkuruzinza anawakilishwa na mawaziri wake
Rais wa Burundi Pierre Nkurunzinza hatohudhuria mkutano huo wakati akisubiria matokeo ya uchaguzi wa ubunge uliofanyika tarehe 29 Juni na badala yake amewakilishwa na mawaziri wa mambo ya nje na wa mambo na ndani pamoja na waziri wa Afrika mashariki na msemaji wa rais.
Viongozi wa Rwanda na Kenya pia hawahudhurii kikao hicho, badala yake wanawakilishwa na mawaziri wa mambo ya nje.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728