12 Julai 2015

ATM ya Maji yazinduliwa Kenya

Maji ya ATM nchini Kenya
Wakazi wa kitongoji duni cha Mathare katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi, sasa wanaweza kupata maji safi ya kunywa na kwa matumizi mengine.

Mpango unaoungwa mkono na serikali umezinduliwa kwenye mji mkuu wa Kenya Nairobi unaowawezesha watu wanaoishi kwenye mitaa ya mabanda kununua maji kwa kutumia kadi.
Vituo vya kuuza maji vimebuniwa kote katika sehemu za mabanda ambapo wenyeji hutumia kadi zilizo na pesa kununua maji safi na kwa bei nafuu.
null
Maji ya ATM nchini Kenya
Wenyeji wa mitaa ya mabanda nchini Kenya wamekuwa na tatizo la kupata maji safi ambapo hulazimika kununua maji kwa bei ghali kutoka kwa wauzaji au kutoka kwa magenge ambayo hudhibiti na kuuza maji hayo kwa kuyachuuza.
Mradi kama huo umefaulu katika baadhi ya maeneo ya vijijini nchini Kenya, lakini hii ni mara ya kwanza kuzinduliwa katika mji huo mkuu.
null
Maji ya ATM nchini Kenya
Vituo hivyo vya kutoa huduma hiyo ya maji vimefanikiwa kutokana na ushirikiano kati ya serikali ya mitaa nchini Kenya na kampuni ya maji ya Grundfos ya Denmark.
Kampuni ya kusimamia huduma ya usambazaji maji, ina mikakati ya kuhakikisha kuwa huduma hii walioianzisha itasambazwa kote katika mji mkuu wa Nairobi na kwengineko nchini humo.
null
Maji ya ATM nchini Kenya
Huku hilo likianzishwa wakaazi wa mitaa kadhaa mjini Nairobi bado wanalalamikia ukosefu wa maji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728