16 Julai 2015

Picha ya kwanza kutoka sayari ya Pluto

Picha ya sayari ya Pluto
Picha ya kwanza inaonyesha kwa undani sayari ya Pluto ilivyo imeonyeshwa kwa mara ya kwanza duniani.

Picha hiyo imepigwa na chombo kisicho na binadamu kilichotumwa kwenye safari hiyo ambacho kilisafiri umbali wa kilometa bilion saba na tano.
Chombo hicho jana jumanne kilitua kwenye sayari hiyo .
Katika mkutano na waandishi wa habari katika chuo Kikuu cha Johns Hopkins kilichopo Maryland Marekani, Mkuu wa utafiti wa sayari hiyo Alan Stern hakusita kuonyesha furaha yake.
"Jana ilikuwa ni siku nzuri na ya kipee kwangu, vipi kwenu."
Mkuu huyo wa utafiti - Alan Stern amesema chombo hicho cha anga kimekusanya taarifa nyingi kutoka kwenye sayari hiyo
"Sawa chombo chetu cha New Horizons kimekwenda sasa zaidi ya mile milioni moja.Zaidi ya kilometa moja na nusu upande wa pili wa Pluto, hivyo ndivyo tunavyokwenda kwa haraka tumefikia karibu na sayari hiyo hapo jana asubuhi. Chombo chetu cha anga kipo katika hali nzuri, kinafanya mawasiliano na dunia kwa mara nyingine mara kwa mara kwa masaa kuanzia asubuhi saa 11 na dakika 50. Tayari tumepata data kutoka kwenye vifaa vya kisayansi vipatavyo vitano, na tutatoa taarifa kuhusu matokeo tuliyopata, lakini ukweli ni kwamba tunachunguza kwa undani , kuna mengi." Amesema Alan Stern.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728