28 Julai 2015

Obama awaonya viongozi wa Afrika

Obama -AU
Rais wa Marekani Barrack Obama,amewasuta viongozi wa Afrika ambao wanaendelea kusalia madarakani hata baada ya
katiba kutowaruhusu kuendelea kuwania tena wadhfa wa urais.
Katika hotuba ya kwanza ya rais wa Marekani kwa muungano wa Afrika katika makao makuu ya umoja huo mjini Addis Ababa,amesema kuwa Afrika haitapiga hatua iwapo viongozi wake watakataa kuondoka madarakani baada ya muda wao kuisha.
Amemtaja hayati Nelson Mandela wa Afrika Kusini, ambaye alikaa madarakani kwa muhula mmoja tu wa miaka mitano na anafahamika pakubwa kote duniani huku akiheshimiwa kama kigogo wa bara Afrika, tofauti na marais wengi wanaoendelea kukwamia madaraka.
Ameongezea kuwa wakati waandishi wanapofungwa huku wanaharakati wakitishwa,demokrasia huwepo tu kwa jina.
Akimnukuu shujaa Nelson Mandela akisema kuwa unapoheshimu uhuru wa wengine watu wote huwa huru.
Amesema kuwa ishara kuu ya maendeleo katika taifa ni vile linavyowachukulia wanawake wake.
Obama
Amewaambia viongozi wa Afrika kwamba maendeleo ya bara hili yanategemea demokrasia,uhuru na haki za kibinaadamu.
Anasema kuwa muda umewadia wa kubadilisha mtizamo wa Afrika kama bara duni lenye kulemewa na umaskini na mizozo.
Aidha amepongeza umoja wa Afrika AU na shirika la Umoja wa mataifa katika mapambano dhidi ya makundi ya wapiganaji wa kiislamu kama vile, Boko Haram kaskazini mwa Nigeria na Al - Shaabab Afrika mashariki.
Amemtaja hayati Nelson Mandela wa Afrika Kusini, ambaye alikaa madarakani kwa muhula mmoja tu wa miaka mitano na nafahamika pakubwa kote duniani huku akiheshimiwa kama kigogo wa bara Afrika, tofauti na marais wengi wanaoendelea kukwamia madaraka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728