02 Mei 2015

Bolt kushindana na Gutlin wa Marekani

Usain Bolt hana tatizo la kushindana dhidi ya Justin Gatlin kwa kuwa anahisi kwamba marufuku ya miaka minne aliyopewa ilikuwa ya haki.

Bingwa huyo mara mbili wa michezo ya Olimpiki hivi majuzi alilalama kuhusu mwanariadha mwengine wa mbio fupi kutoka Marekani Tyson Gay ambaye alipigwa marufuku kwa mwaka mmoja baada ya kupatikana amekula dawa za kusisimua misuli.
''Marufuku aliyopewa Tyson ilikuwa haitoshi na kutuma ujumbe mbaya'', alisema Bolt. ''Justin Gutlin alipigwa marufuku na akaihudumia kwa hivyo sina shida naye'',.
Mkimbiaji huyo wa mbio fupi kutoka Jamaica atapambana na wawili hao wikendi hii katika mbio za 4 mara 100 katika mashindano ya relay huko Bahamas.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728