11 Mei 2015

Korea Kaskazini yazindua Silaha kali

Korea Kaskazini yazindua Silaha kali
Serikali ya Korea Kusini inasema inaamini kuwa Korea Kaskazini inaweza kumiliki nyambizi kadha za kufanya mashambulizi kutoka baharini ndani ya miaka mitano inayokuja.

Hii ni baada ya Korea Kaskazini kuchapisha picha zilizomuonyesha kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Un akitazama majaribio ya kuizindua nyambizi hiyo.
Korea Kusini imezikagua picha hizo za uzinduzi kwenye vyombo vya habari vya Korea Kaskazini na kusema kuwa ni za kweli.
Korea Kusini ilisema kuwa uzinduzi huo ni suala linalochukuliwa kwa umakini na tahadhari kubwa sana.
Sasa Korea Kusini na Marekani zinafikiria kuweka ngao ya mitambo ya kuzuia makombora kutoka Kaskazini hatua itakayogharimu mabilioni ya pesa.
Korea Kusini ilisema kuwa uzinduzi huo ni suala linalochukuliwa kwa umakini na tahadhari kubwa
Hata hivyo haijulikani ikiwa makombora yanayofyatuliwa na nyambizi hiyo yana uwezo wa kubeba silaha za nuklia
Wadadisi wanasema kuwa Korea Kuskazini inaonekana kufanya mambo kwa kasi zaidi kuliko ilivyokisiwa kuunda zana zilizo na uwezo wa kushambulia kwa haraka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728