Manchester United ilitawala mechi lakini ikafungwa bao moja katikati ya kipindi cha pili baada ya mkwaju wa adhabu wa Chris Brunts kumgonga mchezaji mwenza Jonas Olson na kuingia wavuni.
Hatahivyo Manchester United ilitarajiwa kusawazisha baada ya kupata penalti lakini mkwaju huo wa mshambuliaji Robin Van Persie ulipanguliwa na kipa wa West Brom.Van Persie alikosa bao jingine baada ya kipa kuokoa mkwaju aliopiga.
Kwa sasa Manchester United iko juu ya Liverpool kwa pointi nne pekee katika nafasi ya nne.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni