06 Aprili 2015

Mwigizaji Jack Wolper Ashutumiwa Kumsahau Aliyemtoa Kisanii Katika Tasnia ya Filamu Bongo

Mwigizaji Jack Wolper Ashutumiwa Kumsahau Aliyemtoa Kisanii Katika Tasnia ya Filamu BongoUbuyu Mpya Kutoka Instagram kwenye page ya mrekebishatabia kuhusu Mrembo Mwigizaji Wolper Kumsahau aliyemwingiza katika Tasnia ya Filamu:

'HISTORIA: Je unajua aliyemtoa kisanii Jackline Wolper mpaka kupata umaarufu nchini ni nani? Ni mdada mkali wa wa siku nyingi kwenye masuala ya sana Lucy Komba ambaye hivi sasa anaishi na familia yake nchini Denmark.


Alikutana nae kwenye ofisi moja bongo akamuomba namba ya simu walipoachana baada ya kama dk 10 akamuandikia msg anaomba amsaidie kwenye sanaa awe kama yeye Lucy Komba , Jackline alikuwa na saloon ya nywele kipindi hiko baadae saluni ya Jackline Wolper ilifungwa sababu ya kushindwa kulipa kodi, ikafikia hatua akauza gari yake na akaanza kutumia gari ya Lucy Komba... anam-drive Lucy kazini anatumia gari jioni anarudi kumfuata kazini... mambo yakawa magumu kwa Jackie mpaka akauza vitu vya saluni, wakati huo ndo Lucy kwa bidii anamfundisha jinsi ya kuigiza...mpaka baba watoto wa Lucy akawa anamuonea huruma Lucy kumtaka apate muda apumzike!! Haikuishia hapo Lucy akamuunganisha kwenye filamu akawa anaharibu wadau wanamlaumu Lucy kuwa Jackie atoke maana hajui lakini akamtetea na kuendelea kumfundisha mpaka akacheza vizuri.

Filamu za Lucy mbili ya kwanza ilikuwa inaitwa AMA ZAKO AMA ZANGU ya pili KIPENZI CHANGU  baada ya hapo Irene Uwoya akampigia simu Lucy kumuuliza kama ana mtu anataka kufanana naye. Lucy akampigia Jackline na kumwambia akaonane nae na Kanumba na Ray wakaridhia ndo wakamchezesha ile scene ya Ophra baada ya hapo akaanza kudai Ray ndo amemtoa kwenye sanaa kwa ile scene moja aliyocheza.

Lakini baada ya watu kumponda ndo akabadilika na kusema Lucy ndo kamtoa na mpaka leo ndo kisa cha watu kumfahamu Jackline Wolper.... kuumbe Lucy ndo kakufikisha hapo @wolperstylish?? Kila mmoja ana mahali alianzia lkn jaribu kukumbuka Wema hata kama ni kidogo...Halafu jinsi alivyo hata harusi yake hukuudhuria ukaishia kuiponda!! Watu hawakumbuki walikotoka aisee'

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU
KUWEKA TANGAZO LAKO HAPA NI BEI NAFUU

TANGAZO LA KAZI -Commited youth agricultural organisation CYAO is looking for a person who is specialised in agriculture

POSITION DESRIPTION;

Agricultural Technician

Qualifications

Diploma in agriculture

Mode of application applicant must send an updated Cv,birth cirtificate,one recent passport size, an accademic cirtificate, age limit 20 to 35

apply to Project cordinator,Commited youth agriculture organisation,P.O.Box 78438 Dar es salaam or you can call through +255657990920/+255754823728