Inakisiwa kwamba zaidi ya watu hamsini wameuawa katika makabiliano makali mjini humo katika kipindi cha masaa ishirini na manne yaliyopita.
Majeshi ya muungano yakiongozwa na Saudi Arabia kwa siku ya kumi na moja leo Jumatatu, yanaendelea kushambulia ngome za wapiganaji wa Houthi.
Kusini mwa Yemen waasi wa Huthi wamepata mafanikio zaidi dhidi ya wanajeshi watiifu kwa Rais Abdrabbuh Mansur Hadi, kwenye mji wa Aden, licha ya kuendelea kwa mashamambulizi ya angani.
Kazkazini zaidi mwa nchi hiyo, ndege za majeshi ya muungano zimeendelea kushambulia maeneo karibu na mji mkuu Sanaa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni